WELCOME !

THANK YOU FOR VISITING THIS SITE. I HAVE BEEN USING BOTH SWAHILI AND ENGLISH LANGUAGE TO EXPRESS ISSUES - I HAVE ATTACHED ENGLISH VERSION TO SOME OF THE SWAHILI NEWS/STORY AT THE END.

Monday 22 May 2017

KUENDELEA KUKUA KWA UHALIFU MTANDAO - NANI WA KULAUMIWA?

Kumeendelea kukua kwa uhalifu mtandao maeneo mengi duniani – Huku baadhi wakitafsiri hili linatokana na wana usalama mtandao kuonekana kulemewa (Kuzidiwa) na wahalifu mtandao.

Hili limepingwa katika kikao kilicho kamilika mwishoni mwa wiki iliyopita, Nchini Afrika kusini ambapo binafsi nilishiriki na kuzungumza na wenzangu kuhusiana na namna sahihi ya uchunguzi wa makosa ya kimtandao – Kubwa nililozungumzia ilikua ni kuwa rudisha wenzangu kwenye mstari kwa kuwakumbusha juu ya taratibu tulizojiwekea na zinazo takiwa kufatwa na mataifa yote duniani.

Pamoja na mambo mengine, nilikumbusha umuhimu kuhakiki hatua zote za uchunguzi zinakua katika maandishi – Zaidi, nilicho zungumza pia kinaweza kupatikana katika Habari inayoweza kusomeka “HAPA”

Kuhusiana na ukuwaji wa uhalifu mtandao kila mmoja wetu amekiri hili halisababishwi na wana usalama mtandao  kuzidiwa nguvu – Lawama imeonekana kuelekezwa kwa mataifa mbali mbali pamoja na watumiaji wa mwisho “Users”.



Lawama kwa mataifa mbali mbali – Kila uhalifu mtandao unao jitokeza leo umekua ukitabiriwa kabla na mapendekezo kutolewa na wana usalama mtandao isipokua tu kwa matukio machache sana mfamo, Tukio la ModPOS.

Mataifa kupitia vitengo vyake vya kukabiliana na uhalifu mtandao vilipaswa kufatilia maangalizo na maelekezo yanayo tolewa bahati mbaya sana mataifa mengi yamekua hayatekelezi hili. Mara zote baada yatatizo lililotabiriwa na kutolewa ufafanuzi kujitokeza ndipo vitengo husika katika mataifa vitaonekana kutahadharisha wananchi wake kitu ambacho  wana usalama mtandao tumekubaliana hatua hii ya “Fire fighting” Kuangaika na tatizo baada ya kutokea ndio hasa sababu ya kuendelea kukua kwa uhalifu mtandao.

Tukio la hivi karibuni la uhalifu mtandao aina ya Ransomware ambao kimsingi umedumu kwa muda mrefu na maangalizo yalisha tolewa umetumika kama mfano – Atahri za uhalifu huu (WanaCry) inaweza kuonekana kwenye video hapa chini.


Mapendekezo: Tumekubaliana kimsingi ya kua lazima vitengo vyetu vya kukabiliana na uhalifu mtandao katika mataifa yetu kurudishwa kwenye mstari kwa kukumbushwa kuwa wana jukumu la kutoa tahadhari ya matukio ya kihalifu mtandao kabla haya jotokeza na si vinginevyo.

Pia, Tumekubaliana kimsingi kukuza ushirikiano wa kuhabarishana taarifa za kiitelijensia, kubadilishana uwezo na mbinu dhidi ya udhibiti wa uhalifu mtandao ambao bado ni tishio kubwa maeneo mengi duniani.

Lawama kwa watumiaji wa mwisho – Mataifa kadhaa yamekua na tabia ya kutahadharisha juu ya uhalifu mtandao, kupitia machapisho na taarifa mbali mbali ila watumiaji wa mwisho wameonekana kutofatilia taarifa hizi – Mfano uliotolewa ni takwimu ndogo zikionekana kwa watu wengi kufatilia taarifa zinazotolewa zenye mlengo wa kuzungumzia chagamoto za uhalifu mtandao na maeneo mengine ya muhimu.

Mmoja wa wazungumzaji alieleza, Unapoweka taarifa mbili moja inayo husisha taarifa ya tahadhari ya jambo muhimu na nyingine kuelezea taarifa ya msanii mkubwa kupaikana na tukio lolote basi wengi wataonekana kufatilia zaidi taarifa ya msanii na kuacha taarifa yenye tahadhari juu ya usalama wao katika mtandao ambao kimsingi una hatari kubwa sana hasa kwa kipindi hiki ambapo kila kitu kimeunganishwa kimtandao.

Aidha, kumekua na mjadala ulio onekana kuwatetea watumiaji mtandao “Users” ambao ulieleza lugha ngumu inayo tumiwa na wafikisha taarifa hizi unaopelekea watumiaji kutoelewa nao unasababisha kukua kwa changamoto ya watumiaji kutozingatia wanacho ambiwa.

Mapendekezo: ELimu ya uelewa (Awareness program) imeshauriwa kutiliwa mkazo na kila taifa ila pia elimu hii lazima ifate misingi saba tuliyo jiwekea mwa 2015, ambapo tulikubaliana kimsingi  ya kua inapaswa kua ya namna nzuri na rahisi kwa kila mtumiaji kuelewa kirahisi – Kitu ambacho mataifa mengi bado yameonekana kutofanyia kazi hili.

Binafsi, Juu ya hili niliwasilisha kwenye wizara yetu (Nchini Tanzania) ya mawasiliano kupitia kikao ambacho nilizungumza na watendaji katika wizara.

PICHA: Kikao cha mapema mwaka huu ambapo nilizungumza na Watendaji Wizara ya Mawasiliano


Pia nimepata fursa ya kuwa na mazungumzo marefu na Mbwana, Ivo Vegter, ambaye ni mwandishi wa vitabu vya usalama mtandao ambavyo baadhi yake nimekua nikivisoma sana pamoja na kutoa wito kwa wawekezaji katika sekta ya usalama mtandao kuwekeza nchini – Tayari kumekua na muitikio kwenye hili.

Aidha, Nimezuru Jukwaa la Deloitte, Mahali nilipo wahi kufanyia kazi Nimefurahishwa na hatua ya Deloitte kuanzisha kitengo maalum kitakacho kabiliana na uhalifu mtandao.

Tukio la tofauti lililojiri katika vikao vilivyo isha ni kutoa fursa ka kujumuika nasi kwa vijana wa umri mdogo waliozidi 30 ili kuonyesha uwezo wao katika kusaidia kupambana na uhalifu mtandao – Hatua hii imenifurahisha zaidi kwani kuwekeza kwenye vijana wadogo wenye uwezo ni jambo ambalo hata nchini Tanzania tayari nimesha lishauri.

Itakumbukwa vijana wengi wadogo wamekua wakionekana kusababisha halifu kubwa za kimtandao zilizo gharimu Nchi kubwa duniani –  Rejea tukio la TalkTalk la Nchini uingereza lililo sababishwa na kijana wa miaka 16.

Kwa ujumla kulikua na mijadala mingi na mirefu iliyo ambatana na kuonyeshana gunduzi mpya katika sekta ya usalama mtandao huku vikao vidodgo vidogo vya pembeni baina ya wanausalama mtandao vikitumiwa kujadili maswala mbali mbali hasa katika kukuza mashirikiano na kubadilishana uzoefu na usaidizi katika maeneo mengi katika kukabiliana na uhalifu mtandao.


Kesho (Jumanne 22 – May -2017) , Nchi ya Kenya napo kutakua na mkutano wa mwaka wa usalama mtandao ambapo nimepewa Heshma kubwa ya kuongoza mkutano huo – Udhibiti – Utambuzi na utayari wa kukabiliana na uhalifu mtandao ndio maeneo makuu yanayo tegemewa kujadiliwa.


No comments:

Post a Comment