WELCOME !

THANK YOU FOR VISITING THIS SITE. I HAVE BEEN USING BOTH SWAHILI AND ENGLISH LANGUAGE TO EXPRESS ISSUES - I HAVE ATTACHED ENGLISH VERSION TO SOME OF THE SWAHILI NEWS/STORY AT THE END.

Sunday 3 June 2018

NAMNA BORA YA KULINDA VIFAA VYA TEHAMA VYA WATOTO



KWA UFUPI: Kutokana na ukuaji wa teknolojia pamoja na muunganiko wa vitu vingi katika mtandao (IoT) vifaa vingi vya watoto vimekua mhanga mkubwa wa uhalifu mtandao – Hii imepelekea kuchukuliwa kwa hutua mbali mbali za kulinda watoto mitandaoni. Andiko hili lina angazia namna bora ya kulinda vifaa vya watoto vya TEHAMA.
-----------------------------------------

Kumekua na matukio kadhaa yaliyo husisha kuingiliwa kimtandao (kudukuliwa) kwa vifaa vinavyo tumiwa na watoto huku wahalifu mtandao wakiunda program tumishi zenye nia ovu ya kukusanya picha na sauti za watoto.

Mfano, kampuni ya V-Tech ambayo inatengeneza vifaa vya TEHAMA vya watoto Ilipata kudukuliwa na wahalifu mtandao ambapo taarifa nyingi za watoto zilijikuta mikononi mwa wahalifu mtandao.

Shirika la umoja wa mataifa linalo husiana na TEHAMA (ITU) limekua na kampeni maarufu ya Kuwalinda watoto mtandaoni – Child online protection (COP) ambayo imeongezewa nguvu na Kampeni nyingine ya wanausalama mtandao ijulikanayo kama siku ya usalama mtandao “Safer internet day” ambazo kwa pamoja zinatoa msaada ingawa kuna kila sababu kwaa wazazi nao kuchukua hatua kuwalinda watoto wao kimtandao.