WELCOME !

THANK YOU FOR VISITING THIS SITE. I HAVE BEEN USING BOTH SWAHILI AND ENGLISH LANGUAGE TO EXPRESS ISSUES - I HAVE ATTACHED ENGLISH VERSION TO SOME OF THE SWAHILI NEWS/STORY AT THE END.

Monday 30 October 2017

IDADI KUBWA YA PROGRAM TUMISHI ZIMEENDELEA KUIBA TAARIFA ZA WATUMIAJI

Nchini Tanzania Matumizi ya TEHAMA yame endelea kukua katika maeneo mbali mbali. Hii ime endelea kurahisisha upatikananaji wa huduma muhimu na kuwezesha watu kuendelea kuwasiliana kwa urahisi.

Viwanda na Taasisi mbali mbali zimeendelea kutumia TEHAMA ili kukuza ufanisi na kufikia watu wengi kwa kipindi kifupi. Miamala ya kifedha, ukusanyaji kodi, pamoja na mawasiliano ni baadhi tu ya mambo yanayo wezeshwa na TEHAMA nchini.

Usalama wa mifumo ya TEHAMA ni moja ya jambo muhimu sana ambapo Tanzania inapaswa kuwekeza ili kujilinda na aina zozote za kialifu mtandao ambazo zinaweza kupelekea huduma muhimu kutopatikana na hatimae uchumi wa Nchi kuyumba.

-------------------
STATISTICS: Tanzania installed 27,000 KMS of optic fiber connecting all regions and it has 7 mobile operators – About 94% network coverage, 85% SIM penetration and 40% internet users.
-------------------
Mkutano mkuu wa mwaka wa wataalam wa TEHAMA nchini Tanzania ulio fanyika mwishoni mwa wiki iliyopita (26 – 27, Octoba – 2017) jijini Dar-es salaam ulipata kujadili usalama mtandao ambapo mada kadhaa zilizo jikita katika kutoa elimu ya namna bora za kuimarisha usalama wa mifumo yetu zili wasilishwa na kujadiliwa.


Binafsi, Nilizungumza na washiriki kuhusiana na namna bora ya kulinda taarifa zinazo patikana kwenye simu zetu na komputa mpakato (Protecting Mobile devises Data) ambapo vifaa hivi vimekua vikitumika katika utendaji wa shughuli za kiofisi na kufanya miamala ambapo taarifa hizo zimekua muhimu kulindwa dhidi yawahalifu mtandao.
-------------------
QUOTE: “Companies today allow Individuals to make use of their own mobile devises to perform their jobs with direct access to organization’s sensitive data – Therefore, Data in our mobile device are very important for the operations and financial well-being of our business.” – Yusuph Kileo.
-----------------------

Kumekua na kawaida ya kusoma barua pepe za ofisini kupitia simu zetu za viganjani, Kufanya kazi za kiofisi kupitia komputa mpakato binafsi tukiwa maeneo mbali mbali huku yote haya yakipelekea kuweka taarifa muhimu za kikazi kua hatarini kuweza kuingia katika mikono ya wahalifu mtandao endapo hatua stahiki ya kuzilinda hazitachukuliwa.

KUTOEA KUSHOTO: Yusuph Kileo (Mjumbe wa bodi ya wakurugenzi AfICTA), Prof. Mike Hinchey (Raisi wa IFIP) , Samson Mwela (Mkurugenzi Mkuu Tume ya TEHAMA), Prof. Rai (Mkuu wa chou kikuu cha zanzibar - SUZA) na Neema Sinare (Raisi wa ISACA)

Aidha, Vifaa hivi vinaweza kuibiwa na taarifa hizi muhimu kuwa katika hatari ya kutumika vibaya. Hivyo umuhimu wa kuzilinda taarifa hizi muhimu ni wajibu wa kila mtumiaji.

Umakini wa Programu tumishi, tunazo zi weka kwenye simu zetu ni wa kuzingatiwa kwa kiasi kikubwa kwani kutokana na chunguzi mbali mbali ambazo tumeendelea kuzifanya katika ngazi ya kidunia, umebaini asilimia kubwa ya program tumishi kua na tabia ya kuiba taarifa za watumiaji na kuzitumia watakavyo.

---------------------
Non-sanctioned applications create a risk to the mobile devises and for enterprises.
October, 2016 – The Top 10 flash App were discovered as Malware.
Feb, 2017 – According to Cisco, 27% of 222,000 assessed applications present a high-risk.
May, 2017 –100’s of Apps investigated were all found with serious Snooping and spying Characteristics.

---------------------




Jitihada mbali mbali zimechukuliwa ikiwa ni pamoja na makubaliano ya mwaka 2014 yaliyo elekeza kila program tumishi kueleza kwa ufupi kila watakacho toa bure kwa mtumiaji na watakacho chukua kwa mtumiaji sanjari na kutoa fursa ya mtumiaji kukubali au kukataa. Aidha, Tuliasa watengenezaji wa Program tumishi kuhakiki wanazilinda ili kutoruhusu wahalifu mtandao kuziingilia na kuzitumia vibaya kwa kufanya uhalifu.


Wazungumzaji wengine walionyesha mapungufu mbali mbali ya kiusalama mtandao yanayo patikana nchini na kuasa taifa kufunga mikanda zaidi.

Kiujumla, Kukuza uelewa kwa watumiaji mitandao kua na matumizi bora, Kuongezea wataalam wetu ujuzi, Kuimarisha mashirikiano katika kudhibiti matukio ya kihalifu mtandao, Kuondoa urasimu usio wa lazima katika kukabiliana na uhalifu mtandao, Kuwa na watu sahihi maeneo sahihi ya kudhibiti uhalifu mtandao, na kua na vifaa sahihi na madhubuti vya kukabiliana na uhalifu mtandao ni miongoni mwa mambo yaliyo onekana kutakiwa kufanyiwa kazi ili kuweza kupiga hatua dhidi ya kukabiliana na uhalifu mtandao nchini.

Matukio ya kihalifu mtandao yanayo kumba taasisi moja hayapaswi kujirudia kwenye taasisi nyingine – huo ulikua wito wangu kwa washiriki wote. Utoaji wa taarifa za kialifu mtandao ili ziweze kupatiwa suluhu ni muhimu pia kwani kuficha taarifa hizi huku matukio kuendelea kuonekana yakijirudia kunaweza kupelekea changamoto za upotevu wa fedha kimtandao kuendelea kukua nahii ina athari kubwa kwa uchumi wa taifa.


Wito ulitolewa kwa vyuo vyetu Nchini kuondokana na mifumo ya kizamani iliyo nyuma na wakati kwa kujitazama upya na kuandaa mitaala itakayo weza kutengeneza wataalam wenye uwezo wa kukabiliana na uhalifu mtandao nchini.

No comments:

Post a Comment