WELCOME !

THANK YOU FOR VISITING THIS SITE. I HAVE BEEN USING BOTH SWAHILI AND ENGLISH LANGUAGE TO EXPRESS ISSUES - I HAVE ATTACHED ENGLISH VERSION TO SOME OF THE SWAHILI NEWS/STORY AT THE END.

Thursday 30 July 2015

KONGAMANO LA C2C LAKAMILIKA – USALAMA MITANDAO WAJADILIWA SIKU ZOTE MBILI

Nchi ya Tanzania ya bahatika tena kwa mara ya tatu kua mwenyeji wa mkutano wa “Connect 2 Connect” ambapo kauli mbiu ya mwaka huu imekua ni Kuunganisha bara la afrika mwambao hadi mwambao. Katika hotuba iliyotolewa siku ya kwanza katika ufunguzi wa mkutano huo ili elezea changamoto kubwa za usalama mitandao na namna unavyoweza kuleta athiri kwa kiwango kikubwa endapo usalama huu mtandao hautaangaziwa macho. Hotuba hiyo pamoja na mjadala nilio ongoza kwa siku ya kwanza unaweza kusomeka na kuonekana kwa “KUBONYEZA HAPA”.

Mkutano huu wa mara hii uliokusanya washiriki kutoka katika mataifa 30 duniani kote  ulihusisha wafanya maamuzi ya juu, watengeneza sera na wadau wengine kadhaa ambapo Mawaziri na Manaibuwaziri  wa Nchi kadhaa wkiwa ni miongoni mwa waliopata kuongoza mijadala pamoja na kuunganisha mawazo katika maswala mbali mbali ya barani Afrika.

Kongamano hili la mwaka huu lililoandaliwa kwa kushirikiana wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia  pamoja na kampuni ya simu ya TTCL limeonyesha mafanikio makubwa sana kwa kuwezesha kauli mbiu ya mwaka huu kufikiwa kwa kiasi kikubwa kupitia mijadala mbali mbali iliyo jadiliwa katia kongamano hili.

Mbali na mada nyingine mbai mbali – Kwa siku zote mbili za mkutano huu mijaadala mizito ya usalama mtandao ilipata kujadiliwa kwa kina ambapo nilipata bahati ya kuongoza mjadala wa siku ya kwanza na kuhutubia kwa siku ya pili juu ya maswala ya usalama mitandao. 

Katika hotuba yangu ya siku ya pili katika mkutano huu nilipata kuangazia hali ilivyo duniani kote na kueleza kwa kifupi kuhusiana na Mkutano mkuu wa mwaka ulioangazia maswala ya usalama mitandao jijini Johannesburg ambapo pia nilihutubia kwa niaba ya Bara la Afrika tulipo kutana wataalam wa maswala haya katika ngazi ya dunia. Zaidi niliweza kuainisha mapungufu makuu tuliyo nayo yanayo sababisha vita dhidi ya uhalifu mtandao kuenekana kutushinda kutokana na uhalifu huu mtandao kuendelea kushamiri.


Msisitizo mkuu nilio toa mbali na kuhimiza ushirikiano na kutumia vizuri wenye ujuzi na elimu hii ya usalama mitandao, Nilipata kuainisha makundi ma nne ambayo ni Mtu binafsi, kundi la Watu ( Wana usalama mitandao), Kampuni , pamoja na serikali na kueleza kuna dhana potofu inayo dhani makundi matatu kati ya hayo manne ndio yenye dhamana ya usalama mtandao na kusahau kabisa kua lazima usalama mtandao uanzie katika ngazi ya MTU BINAFSI.

Nikitolea hili ufafanuzi – Nilielezea mtu binafsi anakila sababu ya kuhakiki usalama wake uko vizuri kwa kuhakiki neno la siri “Password” Matumizi ya salama ya mitandao na kuhakisha kila hatua za kujilinda dhidi ya uhalifu mtandao kama ilivyo katika hali ya kawaida ya kulinda makazi yetu zina angaziwa vizuri kwani  jukumu la kulinda usalama mtandao si la kundi flani la watu pekee.

Nikiwa na waziri wa TEHAMA - BURUNDi
Waziri wa TEHAMA wa Burundi katika mazungumzo yake mkutanoni na baadae tulipo kutana  kwa mazungumzo baina yetu alionyesha dhahiri matumizi mabaya ya mitandao hasa hii ya kijamii ilivyo changia kuyumbia taifa la Burundi huku akiendelea kutoa wito juu ya matumizi salama ya mitandao ya kijamii ili kuweza kuchochea usalama wa taifa lolote duniani – Katika kuumunga mkono nilimpatia mifano kadhaa ya Nchi kama Misri, Libya na nyinginezo ambazo ziliyumba na kuanguka huku sababu kuu ikiwa ni mitandao ya kijamii kuchochea fujo katika nchini hizo.

Niliwa na Waziri wa TEHAMA -  LETHOSO
Nilifarijika kuona Nchi ya LETHOSO pamoja na NAMIBIA kuonyesha dhamira yao ya dhati ya kutaka kujifunza kutoka kwetu kwenye maswala haya ya usalama mitandao na kupongeza hatua nzuri tuliopiga hadi leo. Katika mazunungumzo yangu na Waziri wa TEHAMA wa LESOTHO alinieleza wimbi kubwa na matumizi mabaya ya mitandao nchini mwake ndio limeendelea kua kikwazo na ana mikakati ya kuandaa sera pamoja na sheria mitandao ili kuhakiki ana himili vishindo vya ukuaji wa matumizi mabaya ya mitandao.

Aidha, Kwa upande wa NAMIBIA – Mbali na kunipongeza walionyesha dhamira ya yadhati ya kufanyia kazi ushauri niliotoa katika mkutano huu, huku wakisisitiza kua wanaamini kabisa tatizo kubwa ni upungufu wa ukuzaji wa uelewa juu ya mambo ya usalama mitandao pamoja na serikali nchini afrika kutoona Usalama mitandao ni kipa umbele na wakisahau Uhalifu mtandao unauwezo mkubwa wa kuangusha taifa lolote.


Mwisho, Nitoe wito kwa serikali ya Tanzania na wadau mbali mbali kutambua athari kubwa katika Nyanja zote kuanzia kiuchumi hadi kisiasa zinazoweza kuonekana kama usalama mtandao hauta angaziwa macho ipasanyo. Wakati huu tukiwa tunaelekea uchaguzi mkuu lazima tujue mitandao ya kijamii inaweza kabisa kuyumbisha taifa letu hivyo hakuna budi kuwa na umakini madhubuti katika hili. Tayari nimesha lizungumzia hili mara kadhaa na zaidi unaweza kupitia Andiko linalosomeka kwa “KUBOFYAHAPA”

No comments:

Post a Comment