WELCOME !

THANK YOU FOR VISITING THIS SITE. I HAVE BEEN USING BOTH SWAHILI AND ENGLISH LANGUAGE TO EXPRESS ISSUES - I HAVE ATTACHED ENGLISH VERSION TO SOME OF THE SWAHILI NEWS/STORY AT THE END.

Wednesday 30 July 2014

CHINA YAHOFIWA KUINGILIA MITAMBO INAYO ONGOZA MAKOMBORA YA WA ISRAEL

Wadukuzi wa kichina katika utaftaji wa taarifa zihusianazo na mitambo inayo ongozea makombora yanayotumiwa na wa Israel nchini palestina wamefanikiwa kuingilia mifumo ya wakandarasi watatu wa ki Israel. Wadukuzi hao wa kichina wamefanikiwa pia kupata kujua taarifa za mipango mingine yawa Israel pamoja na taarifa nyingine muhimu za makombora yawa Israel.

Taarifa hii imekua ikipokelewa kwa namna tofauti na makundi mbali mbali yaliyo onyesha hisia zao kupitia mitandao huku baadhi wakihoji kama inaweza kuleta salama katika hali ya mapigano yanayo endelea hivi sasa huko Gaza.

Kwa mujibu wa taarifa inayosomeka "HAPA", imeelza wadukuzi hoa wana uhusiano wa karibu na Jeshi la Uchina. Mwezi wa tano mwaka Huu 2014, Marekani ilitangaza kuwatafuta wadukuzi wa tano wa kichina wakiwashtumu kuingilia mitandao ya mifumo ya kimarekani. Taarifa hizo hazikuweka wazi ni taarifa kiasi gani wadukuzi hao walifanikiwa kuzichukua huku ikisemekana taarifa 700 ndizo zilizochukuliwa na baadae kuaminika huwenda ikawa ni zaidi ya idadi iliyo tangazwa awali.

Kwa mujibu wa mtafiti wa Chuo kikuu cha Kalifonia cha marekani bwana. John Lindsay alipozungumza na "BUSINESS INSIDER" alielezea huwenda udukuzi huo unaambatana na jitihada za wachina kujifunza zaidi maswala ya mifumo ya kuongozea mitambo ya kivita.

Wakati gumzo la Udikuzi huu ukiendelea kujadiliwa, baadhi wamekuwa wakisema ya kuwa wadukuzi wakichina huwenda walivutiwa na mifumo hiyo yawa Israel ya kuongozea mitambo ya kivita baada ya kushinda kwakwe mapigano ya mwaka 2012 dhidi ya wapiganaji wa kipalestina.


Aidha, Kampuni moja ya ulinzi ya Israel iliyohusishwa na sakata hili imesema hapakua na tahadhari yoyote iliyotolewa kwa washirika wao wa kimarekani juu ya hali hiyo ya kiusalama huku akielezea taratibu zimewekwa vizuri ili kuzuia hali yoyote inayoweza kuhatarisha usalama wa mifumo yao.

Wakati huo huo, Mkurugenzi Mtendaji wa CyberESI ,Joseph Drissel alieleza kuwa Nyingi katika taarifa zilizoibiwa zilizuiliwa na Idara ya Marekani. "teknolojia  nyingi za  Arrow 3 hazikutengenezwa na Israel, bali zilitengenezwa na Boeing na makandarasi wengine wa ulinzi wa Marekani," alimweleza Krebs.

"Tulichokifanya ni kuhamisha  teknolojia tuliyokua nayo kwa wamarekani, nao baadae ndipo walipokutwa na tatizo la kudukuliwa kwa taarifa zao. Katika mchakato huo,  pengine katika taarifa zilizo chukuliwa zinaweza kua ambazo hutumika katika mifumo yetu pia. " Alimalizia Bwana Joseph Drissel.

Marekani ime endelea kuishutumu serikali ya Uchina kwa udukuzi wa aina hii ambao pia unahusisha mifumo ya kuongozea ndege za kivita, Mbali na maafisa watano wakichina kushtakiwa mwezi Mei. Pia mwezi Juni, Marekani iliwashtaki wadukuzi wengine wa kichina kama kwenye taarifa inayosomeka "HAPA" inavyo jieleza kwa kirefu.

Kwa upande wake, China imeendelea kukanusha madai haya ya wamarekani na waizrael, huku ikisisitiza ni mbinu za nchi ya marekani kuzitengeneza njia ya kuziba uhalifu wao wa kudukua taarifa za nchi ya china wanzo endelea nao hivi sasa.

Matishio mbali mbali ya kuathiri mifumo ya mimtadao ya wa Israel yameendelea kuonekana kwa kasi hivi sasa. Hivi karibuni Kundi la Anonymous lilitangaza kuongeza mashambulizi mtandao zaidi kwa taifa la israil kufuatia taifa hilo kuendelea kuishambulia Nchi ya palestina huko Gaza. Kenye taarifa iliyoweza fafanuliwa vizuri "HAPA" ilieleza kundi hilo limewataka pia makundi mengine kuunga mkono jitihada hizo ili kufanikisha mashambulizi yake kwa kiasi kikubwa.

No comments:

Post a Comment