WELCOME !

THANK YOU FOR VISITING THIS SITE. I HAVE BEEN USING BOTH SWAHILI AND ENGLISH LANGUAGE TO EXPRESS ISSUES - I HAVE ATTACHED ENGLISH VERSION TO SOME OF THE SWAHILI NEWS/STORY AT THE END.

Sunday 5 October 2014

TUJIKUMBUSHE MATUKIO MAKUBWA MATANO YAKIDUKUZI KATIKA MAKAMPUNI MAARUFU

Tukiwa tupo ndani ya Mwezi wa kuhamasisha uelewa wa matumizi salama ya mitandao, Marufu kama “NATIONAL CYBERSECURITY AWARENESS MONTH” nimeona si vibaya tukajikumbusha matukio muhimu matano ya kiuhalifu mtandao yaliyojiri mwaka huu.

Huku mataifa mbali mbali yakiendelea kujipanga katika mapambano dhidi ya uhalifu mtandao, bado matukio ya kiuhalifu mtandao yameendelea kuitikisa dunia. Yafuatayo ni matukio matano niliyo chagua kuyajadili siku ya leo.

NEIMAN MARCUS

Mwezi wa pili mwaka huu wa 2014, Kampuni ya Neiman Markus ilitengeneza vichwa vya habari baada ya kuingiliwa na wadukuzi wa mitandao waliofanikiwa kuchukua taarifa za wateja wake na kufanikiwa kuzima kila kiashiria ambacho kingeonyesha hali isiyo ya kawaida katika kampuni hiyo.

Awali taarifa zilionyesha ni wateja milioni moja na nukta moja ndio walio athirika  taarifa za kiuchunguzi ambazo zimeandikwa na “BUSSINESSWEEK” zimefafanua tukio hili.

APPLE

Kampuni ya Apple nayo haikubakishwa salama. Moja ya matukio makubwa yaliyojadiliwa na wana usalama mitandao ni pamoja na tukio la wadukuzi mitandao kuingilia, kuchukua na kuzisambaza picha mbaya za watu maarufu kutoka Hollywood ambao walikua wamezihifadhi katika moja ya huduma za Apple maarufu kama iCloud.

Hili halikua tukio zuri kwa Apple pakizingatiwa liliambatana na uzinduzi wa simu zake za iphone 6. Apple walipolizungumzia hili walisema udukuzi ulilengwa moja kwa moja kwa baadhi ya watu maarufu wa Hollywood na si udukuzi wa jumla ambao ungeathiri watumiaji wengi. Kiundani taarifa ya tukio la Apple inapatikana "HAPA"

TARGET

Wadukuzi mitandao waliingilia kampuni ya taget pia ambapo kwa mijibu wa taarifa inayosomeka "HAPA" imeonyesha athari kubwa iliyoikumba kampuni hiyo ambapo udukuzi huo umeigharimu kiasi cha Dola milioni Miamoja na Arobaini na nane.


WAL-MART

Wal-Mart ni moja ya kampuni yenye kuaminika na bahati mbaya wadukuzi walifanikiwa kuingilia na kuiba taarifa ambazo baadae zilipatikana zikisafirishwa kwenda ulaya ya mashariki. Uhalifu huu Wal-Mart walisisitiza kutouzungumzia na mkuu wake wa kitengo cha usalama mitandao kuanisha katika maelezo yake kuwa wanafanya jitihada za dhati kuongeza usalama wa taarifa zake ili kuzuia chochote kinachoweza kuathiri mitandao yake.

HOME DEPOT

Utakumbuka kupitia taarifa inayosomeka "HAPA" nilizungumzia kwa kina tukio la kuingiliwa kwa moja ya kampuni ya kimarekani ambapo ilitengeneza vichwa vya habari baada ya kungundulika wadukuzi mtandao walifanikiwa kuendeleza uhalifu huo kwa miezi mitano hadi walipoweza kugundulika.

Kwa kumalizia, Si vibaya tukaliangalia hili lililozungumziwa Al-hamisi ya tarehe mbili ya mwezi huu wa kumi kama inavyosomeka "HAPA"  yakuwa taarifa za majina, namba za simu na mengineyo ya watu zaidi ya Milioni 76 yameweza kuibiwa na wadukuzi kutoka katika kampuni ya J.P Morgan Chase. Tukio hili limeelezewa kuwa nitukio kubwa la aina yake

No comments:

Post a Comment