WELCOME !

THANK YOU FOR VISITING THIS SITE. I HAVE BEEN USING BOTH SWAHILI AND ENGLISH LANGUAGE TO EXPRESS ISSUES - I HAVE ATTACHED ENGLISH VERSION TO SOME OF THE SWAHILI NEWS/STORY AT THE END.

Wednesday 8 October 2014

“TYUPKIN” YATIKISA MASHINE ZA ATM

Aina hii Malware inayojulikana kama Tyupkin yaleta maafa katika mashine za ATM. Tyupkin imekua ikisambazwa na kundi la wahalifu mtandao kutokea ulaya mashariki na kusababisha pesa nyingi kuweza kutoka kupitia ATM mashine ambapo tayari wataalam wa usalama mitandao kutoka Kaspersky Lab wakishirikiana karibu na polisi wasio na mipaka “Interpol” wamesha anza oparesheni ya pamoja kutafuta chanzo na ugunduzi katika mashine 50 umebainika hadi sasa.




Video inayo onyesha kilichotokea kwenye Mashine Hizo:


Uchunguzi wa kina umeonyesha Mashine zilizo athirika zimekua zikigundulika kuwa na Window XP yenye 32-bit ambayo tayari Microsoft walisha tahadharisha watumiaji wake. Utafiti unaonyesha Mashine nyingi za ATM bado zimeendelea kutumia Window XP ambapo imekua ikirahisisha sana kuingiliwa na wahalifu.


Tahadhari imeendelea kutolewa katika maeneo mengine kwani ingawa kunajitihada za dhati za kukabiliana na Tyupkin bado inaonekana kusambaa katika maeneo mengine mbali mbali duniani na hofu ni kubwa kua huwenda Afrika ikaonekana kua ni enoo jipya litakalo athirika.


Ili kupata kujua zaidi juu ya ya angalizo la Window XP pitia "HAPA" na Taarifa za kitaalam za kujua zaidi juu ya Tyupkin na uchunguzi wake pitia "HAPA"

No comments:

Post a Comment