WELCOME !

THANK YOU FOR VISITING THIS SITE. I HAVE BEEN USING BOTH SWAHILI AND ENGLISH LANGUAGE TO EXPRESS ISSUES - I HAVE ATTACHED ENGLISH VERSION TO SOME OF THE SWAHILI NEWS/STORY AT THE END.

Friday 3 October 2014

MKUTANO WA WATAALAM WA TEHAMA WA NCHINI KENYA WAHIMIZA USHIRIKIANO


Kushirikiana katika maswala mbali mbali ili kuweza kufikia malengo ni jambo kubwa lililopata kusikika katika mkutano mkuu wa mwisho wa mwaka unaoendelea Nchini Kenya unaojadili changamoto mbali mbali za sekta ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano. Swala la usalama katika mitandao limepata kuangaliwa na changamoto mbali mbali katika mijadala Rasmi (Ndani ya Kikao) na isiyo rasmi (tuwapo nje ya ukumbi wa mkutano) zilipata kuangaliwa kwa ukaribu.

Swala uhimu nililo jifunza ni jinsi uhalifu mtandao katika mataifa haya mawili Kenya na Tanzania yanavyo fanyika na kujua ya kua kubadilishana mawazo katika hili litasaidia kujipanga kukabiliana na uhalifu mtandao ambao tayari kwa nchi ya Kenya umeendelea kukua ikiwa bado kwa Tanzania haujaonekana sana huku Kenya Ikijifunza pia ili kuweza kujipanga kabla ya uhalifu usika kuweza kushika kasi.

Namna mbali mbali zinazotumika na wenzetu wa Kenya ambao wameathirika sana na uhalifu mtandao (Mfano: Wakati Mkutano unaendelea – Baadhi ya mifumo mtandao ya serikali iliripotiwa kuangushwa na wahalifu mtandao) kwenye kukabiliana na uhalifu mtandao huku tukiangalia kwa karibu namna ambavyo teknolojia zinazotumika kupambana na uhalifu mtandao katika nchi hiyo zinavyoweza kutoa msaada wa kina kwenye makabiliano na uhalifu mtandao Nchini Tanzania.



Ufunguzi wa Milango katika kushirikiana katika maswala mbali mbali ya TEHAMA kwa ujumla katika mataifa haya mawili huku tukiangalia kwa karibu namna tunavyoweza kuchukulia umakini mapambano ya uhalifu mtandao katika nchi Hizi mbili na Ukanda mzima  sawa kabisa na jinsi hatua mbali mbali zinazochukuliwa dhidi ya mapambano na Ugaidi katika Ukanda huu.

Hii nifursa nzuri kwa wa Tanzania kuweza kujipanga na kujenga tabia ya kukusanya Guru wa maswala ya TEHAMA ili kujadili changamoto mbali mbali na namna tunavyoweza kutumia wataalam wandani kuweza ku ongeza tija kwenye maswala mbali mbali hususan maswala yahusuyo usalama mitandao kwani tulikubaliana kwa pamoja maswala ya usalama mtandao yamekua changamoto kubwa na yamepelekea kutakiwa kupatikana nguvu ya ziada na pamoja kukabiliana nayo kwa kushirikiana ki mawazo na njia mbali mbali zinazoweza kusaidia katika mapambano dhiidi ya usalama mitandao.

Hili linatokana na uhalisia wa kua Uhalifu mtandao hauna kizuizi, Mhalifu anaweza kuwa popote duniani na kufanya uhalifu katika sehemu nyingine yoyote kwa kuleta madhara makubwa sana. Sambamba na hili ni kuwa kila siku teknolojia inakua na aina mpya za uhalifu zinaibuka katika mataifa mbali mbali hivyo kushirikiana taarifa zinaweza kuongeza tija kwenye makabiliano na uhalifu mtandao.


Mwisho Kabisa ni Wito kwa Wataalam wetu wa ndani. TEHAMA inakua kila kukicha na teknolojia kwa ujumla inabadilika mara kwa mara hivyo hatuna budi kuweza kushiriki katika makongamano na mafunzo mbali mbali ya kila mara ili kuweza kujiongezea uwezo wa maswala mapya ambayo yanaweza kutufanya tukaendana na wakati katika maswala ya TEHAMA. Picha zaidi za Mkutano huu zinapatikana "HAPA"

No comments:

Post a Comment