WELCOME !

THANK YOU FOR VISITING THIS SITE. I HAVE BEEN USING BOTH SWAHILI AND ENGLISH LANGUAGE TO EXPRESS ISSUES - I HAVE ATTACHED ENGLISH VERSION TO SOME OF THE SWAHILI NEWS/STORY AT THE END.

Friday 24 July 2015

USHIRIKIANO NI MUHIMU KATIKA UTHIBITI WA UHALIFU MTNDAO

Itakumbukwa Mwishoni mwa mwezi wa tano mwaka huu katika hotuba yangu niliyo iwasilisha kwa wanausalama mitandao tulipo kutana  jijini Johannesburg mbali na mambo mengine nilihimiza sana ushirikiano baina yetu kwani wahalifu mtandao wameendelea kua mbele yetu kutokana na ushirikiano mkubwa waliokua nao. Ushirikiano unao mabatana na kusambaza vitendea uhalifu mtandao bure auu kwa gharama nafuu mitandaoni.

Baada ya kulizungumza hili laushirikiano wazungumzaji wengine wote walionekana kuniunga mkono na hatimae kuonekana ni swala muhimu lakufanyiwa kazi mapema. Nafarijika kuona Uingereza tayari mukuu wake wa CERT ametilia mkazo kauli hii (Ya ushirikiano) kupitia kikao kilicho malizika London ambapo taarifa kamili kuhusiana na hili inaweza kusomeka kwa “KUBOFYA HAPA”

Aidha, Marekani na Israel baada ya kutia saini makubaliano ya kuboresha ushirikiano katika maswala ya usalama mitandao paliambatana na kuhimiza mataifa mengine kuona umuhimu wa kushirikiana katika vita hii ya uhalifu mtandao.

Nilipata kuzungumza tena katika mkutano wa wanausalama Nchini Cyprus ambapo pia nilizungumza kwa mara ya kwanza kuhusiana na ushirikiano huku nikipongeza umoja wa ulaya kwa kuungana kwao katika hili la usalama mitandao kupitia chombo chao kiitwacho ENISA kinacho hudumia mataifa yote yaliyo ndani muungano wa nchi za ulaya katika maswala ya Usalama mitandao.


Tayari kume endelea kuonekana jitihada mbali mbali zikifanyika kupitia majukwaa yetu ya kimtandao ambapo tunajadili mambo mbali mbali na kuu limekua kukumbushia ushirikiano huku wengi wakionekana kuelezea wazo hili la ushirikiano nililo litoa mkutanoni limeendelea kusikilizwa na mataifa makubwa huka mataifa mengine yakihamasishwa kuiga mfano.

Tanzania kumekua na Kauli kama Umoja ni nguvu, Kidole kimoja hakifunji chawa, Umoja ni ushindi na nyinginezo zinazo hamasisha ushirikiano katika nyanja mbali mbali lakini katika hili la kuunganisha nguvu katika maswala ya uthibiti wa uhalifu mtandao bado naona safari ni ndefu.

Nalisema hili kwa sababu bado uhalifu mtandao unaendelea kukua na ki uhalisia vitengo vinavyo husika na hili nchini bado vimekua havionekani kuungana na kua na uwezo mmoja madhubuti kwa kuhimili uhalifu huu. Kuungana ninaotegemea mimi ni pamoja na kushirikiana katika taarifa, Vitendea kazi pamoja na wataalam ambapo kwa ujumla wake yote matatu yame gawanywa inayopelekea kuto onyesha matunda tegemewa.

Nitatolea mfano uhalifu mpya uliokuja kwa kasi nchini aina ya Clickjacking; wengi wamonekana kuathirika huku athari ya uhalifu huu baada ya kujaribu kujadiliana na wngine wameweza kueleza athari kubwa ipo kwa Tanzania na isipo angaziwa baadae inaweza kuibua uhalifu mwingine ambao utakua ni matunda ya huu ulioko sasa na pengine kua na madhara makubwa sana kwa taifa kiujumla.

Nitoe wito katika hili kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii kufahamu ya kua hawana buni kuhakiki wanaendelea kua na tabia ya kujijengea ulinzi katika ngazi ya mtu binafsi mtandaoni huku wakiwa makini sana na kutafakari sana kabla ya kuandika “THINK BEFORE YOU INK” huku umakini na kubadilisha maneno ya siri kua ni moja ya tabia ya watumiaji mitandao kwani neno la siri madhubuti na linalo badilishwa itakikanapo husaidia kuzuia uhalifu wa udukuzi.

Matumizi salama ya mitandao ya kijamii na kutambua utumiapo mtandao wa kijamii kusemea wengine vibaya au kutumia lugha zisizo rafiki kwa wengine inasababisha uhalifu aina ya Cyberbulling ambao umeendelea kugharimu sana uhai wa watu duniani kote.kuendelea kuangaza macho kwenye mifumo yetu yote ya digitali pia ni muhimu sana kwani ukuaji wa matumizi ya digitali katika maisha yetu lazima tujue yanakuja na changamoto za ukuaji wa uhalifu mtandao hivyo hatuna budi kuongeza umakini katika usalama mitandao.


Faragha zetu katika mitandao ya Kijamii nazo ni zakuangaliwa sana kwani baadhi ya malalamiko ya kihalifu mitandao inatokana na faragha kua na mapungufu ambapo inatoa fursa kwa wahalifu mtandao kupata taarifa za watu binafsi mitandaoni kirahisi sana. Hili linapelekea wengine kutumia mapungufu hayo kutengeneza mitandao ya kijamii feki yenye taarifa za watu wengine na picha zao walizo zipata kupitia mitandao ya kijamii iliyo wazi (faragha dhaifu).

1 comment:

  1. Rose Day, Propose Day, Chocolate Day, Teddy Day , Promise Day, Hug Day, Kiss Day, Valentine's Day, Stickers are unique you will NOT find these stickers anywhere else.Once you start using them you will fall in LOVE with them.Application is friendly and easy to use,it runs smoothly..You can follow us on http://www.facebook.com/valentinespecialstickers


    Love Stickers

    Valentine Stickers

    Kiss Stickers

    WeChat Stickers

    WhatsApp Stickers

    Smiley Stickers

    Funny Stickers

    Sad Stickers

    Heart Stickers

    Love Stickers Free Download

    Android Apps Love Stickers

    ReplyDelete