WELCOME !

THANK YOU FOR VISITING THIS SITE. I HAVE BEEN USING BOTH SWAHILI AND ENGLISH LANGUAGE TO EXPRESS ISSUES - I HAVE ATTACHED ENGLISH VERSION TO SOME OF THE SWAHILI NEWS/STORY AT THE END.

Friday 5 February 2016

SINGAPORE YAFIKIA PAZURI KATIKA USALAMA MTANDAO

Ikiwa bado Singapore inaendelea na mkakati wake wa kua “Smart Nation” imeanisha kuweza kufikia hapo lazima swala la usalama mitandao liwe muhimu zaidi “Top priority”. Hii ni kutokana na uhalisia kua Nchi inapokua ya kisasa zaidi na kutumia kwa wingi mifumo yaki Teknohama katika maeneo mbali mbali uhalifu mtandao nao unaongezeka.

Mwaka jana (2015) katika kuliendea hili la kuhakiki Usalama mtandao unashika nafasi ya juu kwa taifa hilo linalokua kwa kasi barani Asia, Wali anzisha wakala wa usalama mtandao “Cybersecurity Agency” ambapo uliiunganisha vitengo vyote vidogo vya usalama mitandao na kukuza ushirikiano na sekta binafsi nchini humo.

Hatua hiyo ilipongezwa na wana usalama mitandao Duniani kote na binafsi kuliandikia katika andiko linalosomeka “KWA KUBOFYA HAPA”. Tayari nchi hiyo pia ina mpango wa kimkakati wa miaka mitano wa kitaifa wa usalama mtandao “National Cybersecurity Master plan” ambapo inategemewa kuwekeza zaidi katika kulinda miundo mbinu yake ya TEHAMA pamoja na taarifa zake pamoja na Wananchi wake.

Nchi hiyo ya Singapore haikukomea hapo tayari imesha boresha mashirikiano yake na Nchi nyingine za barani Asia ambapo makubaliano maalum kwa nchi hiyo (Singapore), Japan, India na Malaysia ya kuimarisha  zaidi ushirikiano ya kimkakati yameshawekwa mapema mwaka huu (2016) ili kuhimili vishindo vya uhalifu mtandao.


Nguvu hii ya pamoja ya kushirikiana kukabiliana na uhalifu mtandao ni hatua ya Muhimu kwa Nchi hizo za barani Asia – Tayari hadi sasa tumeshuhudia mafanikio mengi kwa nchi za Umoja wa Ulaya (EU) kutokana na hatua za kuunganisha nguvu katika mashirikiano ya pamoja na ya dhati kukabiliana na uhalifu Mtandao.

Kampuni ya Usalama mitandao ya FireEye, Imeainisha Nchi hiyo kua na uwezo mkubwa zaidi barani Asia kukabiliana na uhalifu mtandao. Ingawa bado Nchi hiyo aliiaswa na kampuni hiyo kufunga mkanda zaidi kwani Wimbi kubwa la uhalifu mtandao bado limeendelea kuzitesa Nchi zenye uwezo mkubwa wa kiulinzi mtandao na kuitolea mfano Nchi ya Marekani.

Katika taarifa ya FireEye, Inaeleza Wahalifu Mtandao wameendelea kuitesa Marekani na kuifanya Nchi hiyo kuendelea kuongeza nguvu zaidi kukabiliana na wimbi kubwa uhalifu mtandao. Hivyo Nchi ya Singapore lazima Iendeleze jitihada zaidi kuendelea kuimarisha usalama mtandao wa Taifa hilo.

Ikumbukwe mataifa sasa yame imarisha zaidi si tu mifumo yao ya usalama mitandao bali hata majeshi ya kiusalama mitandao ambayo yameendelea kutumika kuibia mataifa mengine taarifa muhimu na kukabiliana na aina yoyote ya vita mtandao.

Tulipofikia sasa Mataifa mengi yamekua hayapeleki watu wake kwenye Nchi nyingine kwa nia ya kupata taarifa mbali mbali ambazo ni muhimu na badala yake wameendelea kujiimarisha kwenye njia mbali mbali za ki TEHAMA zinazo weza kufanikisha hili pasi na kumueka yeyote kwenye hatari ya kukamatwa katika Nchi ya Kigeni.

Tumeshuhudia hili kwa mataifa kama China, Marekani, Urusi, Korea na kwenginepo. Hadi sasa mataifa Takriban 50 yana nguvu za kihalifu mtandao za kitaifa “offensive cyber capabilities”. Wataalam wa usalama mitandao tumeendelea kusisitiza kua na nguvu hii na kuweza kudhuru Nchi nyingine kimtandao “Cyber Espionage” ina uwiano sawa na ugaidi mtandao.

Hadi sasa Katika mataifa hayo 50 yaliyo jiimarisha ki nguvu mtandao kuweza kudhuru mataifa mengine Singapore si miongoni mwao – Mkurugenzi wa TEHAMA wa  Kampuni ya kiusalama mtandao ya “DarkTrace”  imelishauri taifa hilo (Singapore) kujipanga kwenye hilo na kuhakiki imekua na Jeshi mtandao ili kuweza kukabiliana na taifa lolote litakalo weza kuhitaji kudhuru taifa hilo kimtandao.

Hii ni  kutokana na Mikakakati yake pamoja na ukuwaji wa taifa hilo kwa kasi huwenda mbeleni Baadhi ya mataifa yakawa na dhamira ya kuidhuru Nchi hiyo kimtandao. Marekani kwenye Taarifa inayosomeka “KWA KUBOFYA HAPA” ime eleza wazi iko tayari kivita Mtandao na Nchi Yoyote.

Na Kwa Mara ya kwanza katika historia ya udukuzi, Kampuni ya Kichina ambayo kwa muda mrefu wahalifu mtandao wamekua wakitaka sana kufanikisha kuidukua bila mafanikio mwaka huu imewezekana. Taarifa zaidi zinasomeka kwa "KUBOFYA HAPA" Hili pamoja na tukio la wahalifu mtandao kudukua mifumo ya umeme ya Ukraine na kufanikisha kuzima umeme na kusababisha usumbufu na uharibifu mkubwa yametafsiriwa na wana usalama mtando kua wahalifu mtandao wanazidi kuongeza makali kufanikisha uhalifu mtandao maeneo mengi duniani.

TANZANIA:  NINI TUNAJIFUNZA?

Ikumbukwe Serikali ya awamu ya Nne (4) ya Dr. Jakaya kikwete iliwekeza sana kwenye kuimarisha miundo mbinu ya KITEHAMA – Tukaweza kuwa na Mkonge wa Taifa, Ghala la kuhifadia taarifa la Taifa “Natinal Data Center” pamoja na kuchukua taarifa za wana nchi kwenye usajili wa Vitambulisho vya Taifa pamoja na kupigia kura ambapo taarifa hizi muhimu za wananchi wa Tanzania zimehifadhiwa kwenye mifumo ya KiteknoHAMA.

Hayo pamoja na mengine mengi tuliyo shudia na yanayoendelea kuwekewa mikakati ili kuhakiki Taifa la Tanzania linaendelea kujikita zaidi na matumizi ya TEHAMA maeneo mbali mbali yana liweka taifa pia katika hatari ya kuweza kdhuriwa zaidi na Uhalifu Mtandao.

Lazima Taifa kama Taifa liangazie macho swala hili muhimu la usalama mitandao kama kwa umakini wa kipekee ili kuhakiki Maeneo mbali mbali yatakayo tumia mifumo ya TEHAMA yanabaki salama kimtandao.

Wizi wa Taarifa na fedha zinazopotea kupitia Uhalifu Mtandao unaweka taifa lolote katika hali mbaya na kusababisha kuyumbisha Uchumi, Siasa na Nyanja nyingine mbali mbali.

2014, Wakati Mataifa takriban 21 yalipokutana Nchi kujadili maswala ya usalama mitandao, Mengi yalizungumzwa na kuonekana kua hatuna budi ila kuhakiki swala la usalama mtandao linawekewa mkazo. Kwa Ufupi Yaliyosema na kujiri kwenye hilo yanaweza kutazamwa kwnye Video inayo weza kutazamwa kwa “KUBOFYA HAPA”

Nimepitia Moja ya Andiko pamoja na Michango mbali mbali iliyotolowa ambapo linaweza kusomeka kwa “KUBOFYA HAPA” ambapo nimeona kuna mambo kadhaa ambayo bado Ni CHANGAMOTO kwetu kama ifatavyo: -

MOSI, Vitengo vya TEHAMA kwa Ujumla vimeonekana kuwa na uwezo mdogo wa kuweza kufanya kazi yake ipasavyo. Mfano: Yalitolewa maelekezo hivi karibuni na Ofisi ya Raisi ya kuwapo na Vitengo vya huduma kwa wateja katika ofisi na mashirika ya serikali. Kitu ambacho Vitengo vya TEHAMA Nchini vingeweza kua na mwanzo (Bila Gharama yoyote) kwa kuwa na mifumo ya kutumia Mitandao ya kijamii kusikiliza shida mbali mbali za wana Nchi kupitia kurasa rasmi zitakazotoa fursa kwa wananchi kueleza waliyo nayo ili kupatiwa utatuzi.

PILI, Kumeonekana kua na changamoto ya kuwako na wenye uwezo mdogo wa kugeuza changamoto kuwa fursa KITEHAMA ili kufikiwa kwa malengo mbali mbali. Mfano: Wakuu wa TEHAMA wamekua wakionekana kuhofia sana kushirikiana / Kushikisha wataalam wa Ndani kuwasaidia mawazo ya kutatua mambo mbali mbali kitu ambacho mara nyingi husababishwa na Uwezo mdogo wa muhusika na kuhofia sana kuweonekana mapungufu.

TATU, Kumekua na kufanikiwa kutokea kwa uhalifu mtandao Nchini na bahati mbaya zaidi wakati mwingine unadumu bila hatua zozote kuchukuliwa. Mfano: Nilipata kueleza mwanzo kulibashiriwa na wana usalama mitandao kua uhalifu wa “Click Jacking” ungeikumba Tanzania, Uhalifu huo hatimae ulilikumba taifa kutokana na kudumu kwa muda kutokana na kushindikana kua na mpango wa kimkakati kukabiliana na hili mapema kabla hata ya kuathiri taifa.

Hayo ni kwa uchache ingawa Changamoto ni nyingi zaidi ambazo zipo na zina hitaji utatuzi. Katika Hotuba yangu kwa niaba ya Nchi za Afrika Nchini Afrika Kusini ambapo wana usalama Mtandao kutoka mataifa mbali mbali tulikutana pamoja kujadili changamoto na nini kifanyike niliainisha njia rafiki na madhubuti za kufanyiwa kazi ili kupiga hatua katika kuimarisha usalama mitandao.

Hotuba hiyo iliyo ungwa mkono na Wote akiwemo Mkuu wa Wakala wa Usalama wa Nchi ya marekani (NSA) aliyemaliza muda wake na wengine baadae maazimio yaliendelea kufanyiwa kazi na mataifa mengine mbali mbali na tayari matunda ya kuridhisha yameendelea kuonekana.

Nilitolea ufafanuzi kwenye hutuba hiyo na mengineyo yaliyo jiri katika Video hapo Chini ambapo naimani kabisa endapo Taifa la Tanzania lika amua kufanyia kazi basi tutapiga hatua kubwa sana ukizingatia sasa Raisi wa awamu ya Tano, Dr. J P Magufuli ameonyesha dhamira ya dhati ya kuimarisha uchumi wa Taifa letu – Uchumi ambao Kupitia Uhalifu Mtandao unaweza kuyumbishwa na wahalifu mtandao kupitia namna mbali mbali.

                     


KWAKUANZIA, Tuanze na Kufanyia kazi “Right Skillset to the Right Places” tutumie wenye uwezo kwenye maeneo stahiki. Kisha tuendelee kuwaongezea ujuzi wataalam wa ndani kuendana na mabadiliko ya kasi katika Teknolojia “Capacity building” Bila kusahau kuimarisha elimu ya uelewa “Cybersecurity Awareness program” Pamoja na kuimarisha mashirikiano ya ndani “Collaboration”. Bahati Nzuri Sheria Mtandao “Cyber Law”  Imepaikana na inafanya Vizuri.

No comments:

Post a Comment