WELCOME !

THANK YOU FOR VISITING THIS SITE. I HAVE BEEN USING BOTH SWAHILI AND ENGLISH LANGUAGE TO EXPRESS ISSUES - I HAVE ATTACHED ENGLISH VERSION TO SOME OF THE SWAHILI NEWS/STORY AT THE END.

Thursday 25 December 2014

DIT YAFANYA SEMINA ELEKEZI YA UFAHAMU WA MASWALA YA USALAMA MTANDAO

Swala la kukuza uelewa wa matumizi mtandao salama maarufu kama  “Cybersecurity Awareness programs” imekua iki himizwa sana kwani uhalifu mtandao unaweza kupunguzwa kwa kiasi kikubwa sana pale watumiaji watakapo pata ufahamu wa kina wa matumizi salama wa mitandao.

Swala hili limekua liki imizwa sana na mataifa mbali mbali ili kuhakiki matumizi salama ya mitandao yanakuwepo na hatimae kupunguza wimbi kubwa la uhalifu mtandao unao endelea kukua hivi sasa. Katika kuonyesha umuhimu wa swala hili Mwezi Wa Kumi umekua ukitumika kama mwezi maalum wa kukuza uelewa wa matumizi salama katika mataifa mengi. Kujua zaidi katika Hili Fatilia Taarifa inayoweza kusomeka "HAPA" 

Kwa kutambua umuhimu Huo Chuo cha Teknolojia cha Dar-es-salaam (DIT) kiliandaa semina maalum ambapo wanafunzi wa vyuo mbali mbali waliweza kualikwa kuhudhuria semina hiyo ambayo ilikua na lengo la kukuza uelewa wa matumizi salama ya mitandao.


Washiriki ambao walikua ni kundi kubwa la vijana, ambao pia wanachukua idadi kubwa ya watumiaji mitandao nchini waliweza kupata elimu hiyo ambapo nili iwasilisha kwa kufafanua mambo mbali mbali kuanzia uelewa wa nini hasa maana ya usalama mitandao, uhusiano wa matawi mbali mbali yahusuyo usalama mitandao na athari za uhalifu mtandao hadi sasa katika ngazi ya Dunia.

Aidha, niliangazia Hali ilivyo katika bara La Afrika na Juhudi mbali mbali zinazoendelea ili kuweka Bara salama. Huku niki eleza namna mbali mbali wanavyoweza kujilinda na kuwalinda wengine na uhalifu mtandao.

Maangalizo mbali mbali ambayo yanaweza kupelekea kuweza  kuwatenganisha watu wema wanaofanya uhalifu mtandao bila kukusudia na wahalifu halisi wa mitandao niliweza kufafanua.


Katika Semina Hiyo Palipatikana maswali kadhaa kutoka kwa washiriki hao. Pia Niliendelea kutoa wito wa wataalam wengi kujisukuma katika fani hii ambayo kwa sasa mbado ina wataalam wa chache sana na mahitaji ni makubwa kutokana na ukuwaji wa teknolojia unao ambatana kabisa na matumizi makubwa ya TEHAMA katika maisha yetu ya kila siku.


Kwa Picha Na taarifa iliyo andikwa na mwandishi aliye hudhuria smina hiyo unaweza kusoma kwa "KUBONYEZA HAPA"“ 



No comments:

Post a Comment