WELCOME !

THANK YOU FOR VISITING THIS SITE. I HAVE BEEN USING BOTH SWAHILI AND ENGLISH LANGUAGE TO EXPRESS ISSUES - I HAVE ATTACHED ENGLISH VERSION TO SOME OF THE SWAHILI NEWS/STORY AT THE END.

Sunday 13 April 2014

MJADALA: UHALIFU MTANDAO

Nikiwa na Maduhu mara baada ya mahojiano
Kumekua na muendelezo wa mijadala mbali mbali situ nchini bali katika kila pande ya dunia kutokana na hali ya usalama mtandao inavyozidi kuingia dosari kila kukicha. Mijadala hiyo nchini Tanzania pia imeendelea kushika kasi.

 Mwishoni mwa mwaka jana 2013, nilipata mualiko wakuzungumzia kirefu maswala ya usalama mtandao ambapo pia nilipata kuweka mahojiano hayo kupitia moja ya maandiko niliyo andika kupita blog hii kama yanavyoweza kusomeka na kusikika kwenye mada yangu niliyo elezea na kufafanua kwa kina  NAFASI YA VYOMBO VYA HABARI KATIKA KUTOA ELIMU USALAMA MTANDAO ambapo mlango wa muendelezo wa mjadala uliendelea na elimu kuzidi kutolewa. Aidha taarifa inayo husu nafasi ya vyombo vya habari vinavyoweza kutoa mchango mkubwa katika vita dhidi ya maswala mtandao ilinasomeka katika andiko linalopatikana VIJIMAMBO: USALAMA MTANDAO - VYOMBO VYA HABARI 


Napongeza vyombo vya habari nchini kuona umuhimu wa kuelimisha jamii kuhusiana na usalama mitandao kwani kwa kufanya hivyo jamii inaweza kufungua macho na kuona nini umuhimu wa kujiweka salama watumiapo mtandao.



Kwa sasa hali ya usalama mtandao kwa mujibu wa twakwimu imekua ikiongezeka huku aina mpya za kuweza kusababisha uhalifu zikiendelea kugundulika nabado jitihada za dhati zinaendelea ili kuweza kukabiliana na hali ya uhalifu mtandao.
Kwa upande wa mataifa mbali mbali jitihada znaonekana za dhati, hasa nikitolea mifano vikao vya hivi karibuni katika ngazi ya kidunia nilivyopata kushiriki na kupata kuunganisha nguvu na hatimae makubaliano ya msingi kufikiwa ya kuhakiki mwaka 2014 kuwa mwaka wa vitendo kuhakiki panaingizwa katika vitendo yale yanayo jadiliwa.

Natoa wito kwa watanzania kujenga tabia ya kujiweka salama kimtandao kwani athari inayoweza kumpata mtu mmoja inaweza pia kupelekea watu wengine wengi kuathirika kimtandao. Wahalifu mtandao huwa wanacho kitafuta ni upenyo kupita kwa mmoja tu ili kujijengea mlango wa kuingia katika eneo wanalo panga kulidhuru.

Hivyo swala la kuwa salama kimtandao halijalishi uko katika ngazi gani, ni swala la kila raia kujua anapaswa kua salama ili kuweza kuwalinda na wengine. Majadiliano mbali mbali yanaendelea ndani nanje ya nchi huku hatua stahiki za kukabiliana na hali ya uhalifu mtandao ikiendelea kuchukuliwa.

No comments:

Post a Comment