WELCOME !

THANK YOU FOR VISITING THIS SITE. I HAVE BEEN USING BOTH SWAHILI AND ENGLISH LANGUAGE TO EXPRESS ISSUES - I HAVE ATTACHED ENGLISH VERSION TO SOME OF THE SWAHILI NEWS/STORY AT THE END.

Sunday 13 April 2014

TAHADHARI: “HEARTBLEED" BUG TISHIO JIPYA KWA WATUMIAJI MITANDAO



Wana mitandao kote duniani  hivi sasa bado wako katika hali ya taharuki kufuatia wataalam wa ulinzi mtandao kuweka hadharani tishio jipya la mapungufu yaliyo bainika yanayo ruhusu wahalifu mtandao kuweza kuiba maneno ya siri “passwords” na hata taarifa za kadi za ma benki.


“SSL” ambayo nimeifafanua zaidi kwenye chapisho langu linalosomeka WEB SECURITY ni moja ya program/ kiunganishi cha programu inayo aminika kuweza kuficha taarifa mitandaoni ili  kutoonekana kirahisi, ila baada ya kugundulika hivi karibuni ya kuwa  aina hiyo ya program iliyo aminika kuwa salama imeingiwa na mapungufu lukuki na hadi sasa imeweza kutoa athari kubwa kwa watumiaji wengi wa mitandao ya intanet.

Aidha, tayari makampuni mengi yamesha anza kutoa tahaddhari dhidi ya hali hii ya kutisha kiusalama mtandao na kusisitiza watumiaji kuweza kubadilisha maneno yao ya siri “Password” ili kuweza kujiweka katika hali ya amani kwani huwenda wanayo tumia sasa tayari yalisha chukuliwa na wahalifu mtandao.


Hadi sasa makampuni kama “Google”, “yahoo” na “amazon” kumepatikana namna ya kurekebisha hali hiyo na kumekua na makala yanaendelea kuandikwa kuweza kusambaza elimu kwa uma jinsi ya kuji linda na hali hiyo. Zaidi unaweza pitia taarifa hii ya Heartbleed bug  kwa lugha ya kingereza inayo fafanua na nini chakufanya.

1 comment: