WELCOME !

THANK YOU FOR VISITING THIS SITE. I HAVE BEEN USING BOTH SWAHILI AND ENGLISH LANGUAGE TO EXPRESS ISSUES - I HAVE ATTACHED ENGLISH VERSION TO SOME OF THE SWAHILI NEWS/STORY AT THE END.

Tuesday 27 May 2014

KESHO YA UHALIFU MTANDAO SEHEMU YA MWISHO

Katika sehemu ya kwanza ya habari hii inayosomeka "HAPA"  na pia ilipata kusikika kwenye kipindi cha redio cha Teknohama kama kinavyosikika "HAPA" nilizungumzia changamoto za uhalifu mtandao hii leo na kugusia aina mbili za awali za uhalifu mtandao unaotegemea kuongeza kasi hapo kesho. 

Aidha katika sehemu hii ya pili nitajikita katika mifano zaidi ya Uhalifu mtandao hapo kesho , kugusia mapambano yanayoendelea katika kukabiliana na uhalifu mtandao kwa mifano nikianzia na huu unaosomeka  "HAPA" na mwisho nitazungumzia wito wangu kwenye hili ili kuweza kupata taifa, Afrika na Hatimae Dunia salama kimtandao . . . 

Kuingilia kila kinachotumika majumbani, Hili nalo limeanza kuleta wasi wasi mkubwa ya kuwa wahalifu watafikia mahali waweze kuzima au kuwasha taa za majumba ya watu bila wao kuwepo eneo la tukio Si tu kufanya hivyo hii itausisha na kubadilisha vitu mbali mbali ndani ya majumba ya watu pasi na wao kuwepo eneo latukio.

Hili limezungumzwa baada ya kukuwa kw kasi kwa kinacho julikana kama “Smart Houses” ambapo tayari zimesha anza kutumiwa katika maeneo mbali mbali. Nyumba hizi kila kilichomo ndani kina ongozwa na rimoti maalalum ambayo inakua inahusisha mtandao, hivyo wahalifu wanapokuwa wameingilia mtandao wa muhusika wanaweza kusababisha athari niliyo ieleza hapo juu.

Kuingiliwa kwa mifumo ya magari, Inagawa uhalifu huu si mgeni tayari ulisha anza kuleta athari katika baadhi ya maeneo kama taarifa inayosomeka "HAPA"  ilivyo changanua kwa kina aina hii ya uhalifu. Pametabiriwa uhalifu huu kushika kasi zaidi hapo kesho.

Hili limeleta wasi wasi mkubwa sana kwa wataalam wa maswala ya ulinzi mtandao ukizingatia magari mengi yamekua yakiwekewa mifumo ya komputa kuwezesha mambo mbali mbali katika magari hayo. Mapema mwaka huu kulitokea tukio maarafufu lililogundulika pale “Formula One racing team” waliposema wanaamini mfumo wa kuliongoza gari waliyokuwa wanatumia lilikua na virusi.




Tukio hilo lilipelekea kampuni ya “Ford” kuangalia upya magari yake kujua kama kuna mengine yaliyokuwa ya meathirika na virusi na sasa hivi “Ant-virus” za magari ziko mbioni kutengenezwa na inasemekana zitatumika kwa magari yote yenye kutumia mifumo ya kidigitali.

Wizi wa utambulisho wa watu, kwa sasa bado utambuzi kwa njia ya mtu alicho nacho (namaanisha, Macho, vidole na vinginevyo) kutoa ruhusa kwa muhusika kupata huduma au kuingia katika majengo haija shika sana kasi ingawa ndio njia imekua ikiaminika kuwa salama na imeendelea kuonekana kutumika katika baadhi ya sehemu.

Kinachotokea ukusanyaji wa taarifa hizi za watu “Biometric details” unapokamilika uhifadhi wa taarifa hizi huwa unafanyika pasipo salama kutokana na kutokuwa na wizi wa taarifa hizi. Hivi karibuni wasi wasi umeonyeshwa yakua taarifa hizi zitakuwa zikiibiwa ilikuwapa ruhusa wahalifu kuzitumia kufanya uhalifu. Hili tayari lime anza kuingizwa kwenye tamthilia mbali mbali ikiwa ni hatua za kuelimisha jaami dhidi ya uhalifu mtandao.

Mifano hiyo mitano ni baadhi tu ingawa tayari mijadala mbali mbali inategemewa kuanza kujadili hali ya kesho katika maswala ya uhalifu mtandao. Na namna ya kuanza kutengeneza mipango madhubuti ya kukabiliana nao. Hii ni pamoja kila nchi husika kukuza uelewa kwa raia wake kuhusiana na changamoto za uhalifu mtandao na kueleza kama ilivyo kwa uhalifu mwingine kuzuia kunaanzia nyumbani. Taarifa maarufu iliyotolewa na " THE NEW YORK TIMES" imeliainisha hili.

No comments:

Post a Comment