WELCOME !

THANK YOU FOR VISITING THIS SITE. I HAVE BEEN USING BOTH SWAHILI AND ENGLISH LANGUAGE TO EXPRESS ISSUES - I HAVE ATTACHED ENGLISH VERSION TO SOME OF THE SWAHILI NEWS/STORY AT THE END.

Monday 19 May 2014

WASIWASI WA KIUSALAMA MTANDAO WA TANDA KWA WATUMIAJI SIMU ZA ANDROID

Ransomware Gang, imebashiriwa kuleta athari kubwa sana kwa watumiaji wa simu za androids. Kauli hii iliainishwa na mkurugenzi mkuu wa Trend Micro bwana JD Sherry baada ya kunukuliwa akisema mwaka huu wa 2014 watumiaji simu wanategemea kuathirika zaidi kiusalama mtandao huku akionyesha wasi wasi kuwa wateja/watumiaji wa simu hizo hawako tayari (bado hawajajipanga) kukabiliana na changamoto hii ya kiusalama.


Kile kilicho onekana sana kwa watumiaji wa komputa ambapo wahalifu wanazifunga komputa kwa watumiaji makusudi ili kuwataka wahitaji msaada wa kufunguliwa na Ransomware uhalifu huu umegeukia  simu za viganjani hivi sasa kutokana na ukuwaji mkubwa wa watumiaji wa simu za viganjani.

Nini Kinacho tokea?

Mara tu “Reveton mobile” inapo athiri  simu itaonnyesha kwenye simu tahadhari isiyo sahihi ambayo chanzo chake kinaonekana kutokea mahala ulipo / katika nchi unayo patikana zaidi inaonekana inatoka katika chombo cha ulinzi na usalama mahali ulipo – hii imekua na usumbufu mkubwa kwa watumiaji simu.


Palipo hojiwa ni jinsi gani wahalifu wanaweza kujua mahali ulipo? – Bwana Bogdan Botezatu kutoka katika kampuni ya “Bitdefender” inayo jihusisha na ulinzi mtandao maarufu kwa utengenezaji wa “Antivirus” ijulikanayo kama “Bitdefender antivirus” alifafanua na kusema wahalifu hao wanatumia “Geolocation” ambayo inamuwezesha mhalifu kujua muhusika yuko wapi.


Kisha simu hiyo inafungwa/ kujifunga na mtumiaji kupata shida kufuingua hapo ndipo msaada zaidi utahitajika.  Ili mtumiaji aweze kupata simu yake/ kuifungua anahitajiwa kulipia kiasi cha dola mia tatu (300) kwa wahalifu mtandao kupitia njia zisizo weza kugundulika kirahisi pale uchunguzi unavyotakiwa kufanya. Mifano wa njia hizo umetolewa ni Paysafecard au uKash.

Nini chakufanya?

Bado kuna jitihada za dhati kwenye hili ili kupata ufumbuzi ila pia yafuatayo ni vizuri watumiaji simu wakazingatia.

1.       Umakini wa kujitahidi sana kuwa na matumizi salama ya simu zetu za viganjani hasa kwa wale wanaotumia intaneti kuweza kuwasiliana na ndugu jamaa na marafiki pamoja na kupata taarifa mbali mbali.

2.       Kujitahidi kutumia Antivirus katika simu na hakikisha antivurus unayo itumia iko ndani ya wakati (Haijapitwa na muda) nan i salama kwa matumizi.

3.      Jitahidi kuto bonyeza links kwenye simu ambazo zinaonekana haziko salama hasa kwenye mitandao hatarishi.

4.      Jitahidi kujiunga na “wireless network” ambayo ina alama ya ufunguo kwani iko salama vinginevyo unaweza kujikuta kila unacho safirisha na kupokea kinaonekana na wengine. Aidha wigo la wahalifu kukuingilia linaongezeka. – Tazama Mfano wa wireless salma hapo chini kwenye picha.


5.      Marazote unapo pata tatizo la kiusalama mtandao sit u katika simu bali hata komputa jitahidi sana kutoa taarifa katika kitengo kinacho husika na maswala ya ulinzi mtandao ( Kama Uko Ofisini) Na inashauriwa maswala ya kiofisi - hasa yanayo hitaji umakini mkubwa  si vyema sana kuyafanyia kazi kupitia simu yakiganyani pale unapokua mtandaoni.

Taarifa hii pia nilipata kuiandikia kwa lugha ya kingereza kama inavyo someka hapo chini.

No comments:

Post a Comment