WELCOME !

THANK YOU FOR VISITING THIS SITE. I HAVE BEEN USING BOTH SWAHILI AND ENGLISH LANGUAGE TO EXPRESS ISSUES - I HAVE ATTACHED ENGLISH VERSION TO SOME OF THE SWAHILI NEWS/STORY AT THE END.

Tuesday 20 May 2014

WANAOTUMA JUMBE ZA NGONO KUPITIA SIMU KUFUNGWA JELA NCHINI KENYA

Kwa mujibu wa tovuti ya "BBC SWAHILI"  Serikali ya Kenya imesema watu watakaopatikana na hatia ya kutuma ujumbe wa kingono kwa kutumia simu za kiganjani na intaneti watafungwa Jela.

Adhabu hiyo itawahusu wale wanaotuma ujumbe wenye picha za watu walio uchi na zenye mada ya ngono nchini humo.
Maafisa wakuu wa serikali wanasema kuwa yeyote atakayepatikana na hatia atafungwa jela kifungo cha miezi mitatu kwenda chini.

Afisa mkuu kutoka tume ya mawasiliano ya Kenya , Christopher Wambua, ameviambia vyombo vya habari nchini humo ,kwamba watu wenye tabia hiyo ya kutuma ujumbe wa kingono ,pamoja na picha zenye watu walio uchi ,watatozwa hadi shilingi elfu hamsini za Kenya au dola miatano na themanini na nane za kimarekani sawa na shilingi laki tisa arobaini elfu na mia nane za kitanzania kama faini au kufungwa jela.

Onyo hilo litawahusu hasa wale walio na uzoefu wa kutumiana ujumbe kama huo kupitia kwa simu ya kiganjani au kwenye intaneti. 

Kwa mujibu wa taarifa za serikali, kiwango ambacho watu hutumiana ujumbe wenye mada ya ngono pamoja na picha za watu walio uchi, zao wenyewe au za mtu mwingine kwa simu zao za kisasa ilipanda hadi asilimia sitini.

Hatua zilizo chukuliwa na wengine:

Kwa muda sasa nchi kadhaa zimechukua hatua ya kuhakiki wananchi wake hawapati nafasi ya kuperuzi mitandao isiyo endana na maadili ya nchi husika ikiwa ni pamoja na nchi kama China na Saudi Arabia. Wakati huo huo nchi mbali mbali zimeendelea kuhakiki picha zisizofaa mitandaoni hazipatikani kwa watoto hasa walio chini ya miaka 18.


Maswala haya yamekua yakijadiliwa kwa kina katika vikao mbali mbali vya usalama mtandao ikiwa ni pamoja na kikao cha “CYBERSECURITY EVENT” na pia riport ya Dr. Toure wa ITU aliyo itoa “GENEVA PRESS CLUB” ilipata kuainisha changamoto mbali mbali katika swala hili. ITU Haikuishia katika maneno bali  imeweza kutilia mkazo zoezi la "COP" ili kuwalinda watoto mtandaoni ambalo kw sasa lipo katika hatua ya kuridhisha.

Aidha, Wadau mbali mbali wa maswala ya usalama mtandao wamepata kuandikia namna ambayo watumiaji wa “COMPUTER” na "ANDROIDS" wanaweza kuzuia picha zisizo sawa kuwafikia wawapo mitandaoni.
 

  


No comments:

Post a Comment