WELCOME !

THANK YOU FOR VISITING THIS SITE. I HAVE BEEN USING BOTH SWAHILI AND ENGLISH LANGUAGE TO EXPRESS ISSUES - I HAVE ATTACHED ENGLISH VERSION TO SOME OF THE SWAHILI NEWS/STORY AT THE END.

Friday 13 June 2014

KENYA YAWASILISHA RIPOTI YAKE YA USALAMA MTANDAO

Bwana. Joseph Tiampati
Mashambulio ya mtandao nchini Kenya yamekuwa ni zaidi ya nusu kwa mwaka uliopita, na nchi kupoteza takriban shilingi bilioni 2 (dola milioni 22.8) kwa mwaka, hii ni kwa mujibu wa ripoti ya usalama mtandao ya Kenya ya mwaka huu wa 2014.

Ikiwa ni kipindi muhimu ambapo ripoti  za usalama mitandao katika ngazi mbali mbali zinaendelea kuwasilishwa, Kenya nayo imewasilisha ripoti yake ya mwaka 2014 huku ikiwa imeonyesha hofu kuzidi ya ukuaji ma uhalifu katika usalama mitandao  nchini mwake.

Ripori hiyo inayoweza kupatikana "HAPA" imekuja wakati muafaka kwani Kenya ipo kwenye mchakato wa kuboresha sera zake zihusuyo usalama mtandao na kuimarisha uwezo wake wa kupambana na uhali mtandao nchini humo. Ki undani katika hili linasomeka "HAPA"

Akizindua ripoti hiyo, Katibu Mkuu Habari na Mawasiliano na Teknolojia Joseph Tiampati alisema wahalifu, ikiwa ni pamoja na magaidi, wameingia katika mitandao kufanya shughuli za uhalifu, na aliyataka mashirika kudumisha mifumo mizuri ya usalama kulinda dhidi ya mashambulizi.
Bwana. Kris Senanu

Aidha, Bwana Kris Senanu akizungumza katika uzinduzi huo ameeleza yakua Mitandao hii leo imekua ni nyenzo muhimu katika ukuaji wa uchumi na pia kijamii pamoja na kuzitaka kampuni za mawasiliano kuhakiki usalama wa mifumo yao iko vizuri ili kuweza kukidhi mahitaji ya wateja wao.


Ripoti hiyo iliyoandaliwa na Wizara ya Habari kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa teknolojia ya habari na mawasiliano, ilieleza kulikuwa na mashambulio milioni 5.4 ya mtandao yaliyogunduliwa mwaka 2013, ukilinganisha na milioni 2 mwaka 2012, gazeti la The Standard la Kenya liliripoti.

Ripoti ilionyesha kwamba vitisho vikubwa katika usalama wa mtandao mwaka 2013 vilikuwa ni udanganyifu wa wafanyakazi, vitisho vya mawasiliano ya simu, huduma za benki katika mtandao, udanganyifu wa kifedha kupitia simu za mkononi na upelelezi kupitia mtandao.


Idara ya Uchunguzi wa Udanganyifu katika Benki iliripoti shilingi bilioni 1.49 (dola milioni 7) ziliibwa kutoka katika akaunti za wateja mwaka 2013 pekee kupitia mfumo wa udanganyifu uliofanywa na wafanyakazi, kwa mujibu wa ripoti.

No comments:

Post a Comment